Kuongezeka kwa Mwili Wangu Hakujaathiri Chochote katikaKazi Zangu :-Linah Sanga
Mwanadada Linah Sanga amefunguka na kusema kuwa swala la kuongezeka kwa mwili wake baada ya yeye kujifungua hakuathiri kazi zake kwa sababu anaweza kufanya kitu chochote jukwaani kuwafurahisha mashabiki wake,
Hii inakuja baada ya moja ya picha yake ya wikiendi hii kusambaaa sana katika mitandao ya kijamii ikimuonyesha akiwa kama amenenepa sana na kuwa anaweza kushindwa kufanya show nzuri kama zamani,
Akiongea na mtandao wa Clouds fm Linah anasema “mazoezi nayafanya ya kawaida tu, naupenda sana mwili wangu.mimi naona kawaida tu na kuongezeka kwa miwli wangu hakujaathiri chochote katika kazi zangu, napiga show jukwaani na najona mwepesi tu.unajua kuna watu ni wembamba lakin wazito lakini mimi unene wangu haujanipa changamoto yoyote.ninapokuwa jukwaani nawaburudisha mashabiki wangu kama kawaida, lakini ujue pia kuwa mimi sio dansa naimba nitakavyo sio lazima nianze kuruka ruka,’