Lady Jay D Ameongea Haya Kuhusu Nyimbo Zake Kupigwa Stop Kusikika Clouds FM

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’ amefunguka kuhusu nini sababu hasa nyimbo zake kutopigwa na stesheni ya redio ya Clouds Fm.

Miaka kadhaa iliyopita Lady Jay Dee aliingia kwenye bifu kali na mkurugenzi wa vipindi wa Clouds FM, Ruge Mutahaba hali iliyosababisha kukatika kwa uhusiano kati yake na kampuni nzima ya Clouds Media Group hadi kupelekea stesheni kutopiga nyimbo zake tena.

download latest music    

Lakini tangu miaka kumekuwa na maneno Mengi yamekuwa yakiongelewa kuhusu suala hili kwani tangu hapo nyuma hakuna hata nyimbo moja ya Jaydee ambayo inachezwa na Clouds FM. Kila upande ulishaonhea unahitaji msamaha yaani kumaanisha Jide na Clouds, lakini pia Jaydee alishatoa ruhusu ya wao kupiga nyimbo zake hapo nyuma pia.

Kwenye Interview aliyofanya na Dizzim Online Jaydee amesema hajawahi kukataza kituo hicho kucheza nyimbo zake na hata hivyo walisharuhusiwa na Seven lakini hakuna kilichofanyika.

Ilisemekana kuwa mimi ndio nilikataza  nyimbo zangu kupigwa jambo ambalo sio kweli Mimi sikukataza nyimbo zangu kupigwa na hakuna sehwmu yeyote niliyoandika nyimbo zangu zisipigwe, wao ndio waliamua kwasababu kuongea kwangu kule ndio nyimbo zangu zisipigwe. Baada ya hapo alisema akitoa ruhusa nyimbo zake zipigwe zitapigwa Seven akaongeq akatoa go ahead zipigwe je zilipigwa? Kwaiyo hapo sio tatizo langu inaonekaana dhahiri tatizo liko wapi na mtu anaweza kuongea kitu sio kwa kumaanisha”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.