Lady Jay Dee:Nashinda Kutwa Nzima Nikisiliza Kazi Za Aslay

Sio wasanii wote ambao wamekuwa wakifunguka na kusema hisia zao  juu ya kazi za watu wengine tena hasa unapojua kuwa yupo katika kategoria moja ya kazi, hii imekuwa tofauti kwa mwandada lady jay dee ambae si zaidi ya mra moja amekuwa akisifia wasaniiw enzie kwa kazi nzuri wanazokuwa wanafanya.

hivi karibuni akiongea na moja ya magazeti pendwa ya habari nchi, mwanadada lady jay dee amesema kuwa amekuwa akivutiwa sana na kazi anazofanya msanii anaekuja kwa kasi sasa aslya ambae amekuwa akitoa nyimbo kila kikicha na zimekuwa zikifanya vizuri sokoni.

download latest music    

lady jay dee amesema kuwa kuna wakati unakuwa unaitaji kupumzika na kusikiliza muziki mzuri na mara nyingi amekuwa akishinda kutwa nzima akisikiliza muziki wa dogo aslay kwa sababu unamburudisha sana.

mimi ni mwimbaji lakini hii hainifdanyi mimi kushindwa kusikiliza kazi za watu wengine hata kidogo,ninahitaji burudani kutoka kwa wenzangu.kwa mfano ninaweza kutumia muda mwingi sana  wakati mwingine ninashinda hata kutwa nzima nikisikiliza muziki  wa aslay, anajua kuandika na  kuimba  kuimba nyimbo nzuri pia.

Lady jay dee ni mmoja wa wasanii wakongwe ambao wamekuwa katika game kwa muda mrefu na hajawahi kuwa mchoyo wa kusema kil wasanii wengine wanachofanya kama ni kizuri au kibaya.Hii hatakuwa mara ya kwanza kwa msanii lady jay dee kumsifia msanii huyo chipukizi ambae amekuwa akifanya vizuri anapokuwa jukwaani na nyimbo zake zimekuwa zikijulikana kila kona mpaka kwa watoto.

Hata hivyo Aslay ambae amekuwa akitoa nyimbo mfululizo  bila kuogopa kuchuja amesema kuwa kwa sasa amekuwa akitoa nyimbo mfululizo ili kutengeneza  album yake mwenyewe kwa sababu hawezi kuwa akiimba nyimbo za kundi ukizingatia kwa sasa amekuwa akifanya kazi  peke yake.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.