Linah aonyesha muonekano wa kitanda cha mwanae anayemtarijia hivi karibuni

Linah bado hajataja jinsia ya mtoto wake mtarajiwa ila anaonekana ameanza kujipanga mapema kwani amebakisha wiki kadhaa ajifungue.

Muimbaji huyo wa Bongo amekuwa akiposti picha kuonyesha ujauzito wake huku akiwa na furaha ya kuwa mama kwa mara ya kwanza maishani yake. Hata hivyo hajamtambulisha baba ya mtoto anayemtarajia lakini hapo mbeleni aliweza kufunguka kwa kusema kuwa ni mtu wa dini ya Kislamu.

download latest music    

Hata hivyo amebakisha wiki kadhaa ajifungue na kulingana na mtandao wake wa Instagram, Linah ameanza kujipanga kwa kumnunulia mwanae kitanda na doli kadhaa alizoziweka mtandaoni wake.

Tazama picha aliyoiweka hivi karibuni.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua