Linah Ataja Orodha ya Wanaume Aliowahi Kubanjuka Nao

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva, Linah Sanga amefunguka na kutaja idadi ya wanaume ambao ametembea nao tangu amekuwa supastaa na hata kabla hajawa staa.

Linah ambaye kwa sasa ni mama wa mtoto mmoja wa kike anayeitwa Tracey Paris alipata umaarufu miaka ya nyuma baada ya kuanza Sanaa yake kutokea katika jumba la vipaji Tanzania house of talents(THT).

download latest music    

Ingawa Linah kukiri kutulia kwa hivi sasa na mtoto wake na Baba wa mtoto wake, amekiri kuwa miaka ya nyuma kidogo ameshawahi kubanjuka na watu kadhaa ambao kwa sasa wamebaki kama historia tu katika maisha yake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na East Africa Tv, Kikaangoni Linah amefunguka na kutaja kuwa tangu amekuwa maarufu amekwisha wahi kutembea na wanaume watano tu mbali na mwanaume ambaye amezaa naye na anaishi naye kwa sasa:

Kwa haraka haraka naweza kusema nimeshatoka na wanaume watano tu toka watu wamenifahamu kama Linah sina idadi kubwa sana”.

Lakini pia Linah amesema wanaume hao watano ni baada ya kupata jina wakati tayari watu wanamfahamu kama msanii kabla hajajulikana ameshatembea na wanaume kama 10 au 15 ingawa hawakumbuki.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.