Linah: Siko Tayari Kufunga Ndoa

Mwanamuziki wa Bongo fleva Linah Sanga amerudi kwenye ramani ya muziki hivi karibuni na kutoa wimbo wake mpya unaoitwa ‘Same boy’ aliomshirikisha msanii mwenzake Rachel Kizunguzungu.

Linah alikuwa amepumzika kufanya Muziki kwa kipindi kirefu hakusikika hasa baada ya kuwa mjamzito mwaka jana na kujifungua mtoto wake wa kwanza wa kike aitwaye Tracey ambapo alipokuwa mjamzito Linah aliweka wazi kuwa anapumzika kufanya mziki.

download latest music    

Katika kuitangaza nyimbo yake mpya Linah amefanya Interview na kituo East Africa Tv kupitia kipindi cha Kikaangoni ambapo Linah alifunguka na kusema kuwa hana mpango wa kuolewa pamoja na kuzaa mtoto na jamaa yake anayeitwa Shabani au kwa jina jingine Director ghost.

Kwenye Interview hiyo Linah alifunguka na kusema:

Hilo suala la ndoa ni zito yaani ulivyotaja ndoa mpaka nimeshtuka unajua ndoa ni kitu nyeti sana siwezi kukisema tu of course napenda na ninatamani kuolewa mimi ni mtoto wa kike lakini sidhani kama niko tayari kwa sasahivi kuolewa yaani Mungu atusamehe tu tunazaa nje ya ndoa sawa lakini suala la ndoa ni la kujipanga sana”.

Lakini pia Linah amefunguka na kusema Baba mtoto wake yuko tayari kabisa kumuoa lakini yeye ndio hayupo tayari ingawa ameongezea mbali na sababu zote hizo bado kuna mambo yao makubwa yanaowafanya wasioane ambayo wote wanayaju.

Kumekuwa na tetesi kuwa wawili hao hawawezi kufunga ndoa kutokana na tofauti za kidini ambapo Linah ni mkristo lakini mpenzi wake ni muislamu.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.