Linah- Siwezi Kuwa na Mwanaume Asiyekuwa na Hela

Mwanamuziki wa Bongo fleva Linah Sanga amefunguka na kuweka wazi kuwa anapendelea kuwa na mwanaume ambaye ana hela na kamwe hawezi kuwa na mwanaume ambaye hana pesa.

Siku mbili hizi Linah amekuwa aki trend sana kwenye vyombo vya habari na social media hii inatokana na mahojiano anayokuwa anafanya kwa ajili ya kuitangaza ngoma yake mpya aliyomshirikisha Rachel Kizunguzungu inayoitwa ‘same boy’.

download latest music    

Linah amefunguka hayo kwenye mahojiano aliyofanya na East Africa Tv Kupitia kipindi chao cha Kikaangoni ambapo ameongelea sifa za mwanaume ambaye angependa kuwa naye huku akitia msisitizo kwenye suala la kuwa na pesa.

Kwanza mwanaume ambaye naweza kuwa naye awe mrefu kwangu maana mimi ni ka shotii alafu mimi napenda mwanaume mweusi ambaye giant wale wenye miili mikubwa alafu cha pili na cha muhimu awe na pesa ili aweze kunitunza kwa sababu tutake tusitake mtoto wa kike anahitaji kutunzwa sio lazima awe milionea hapana lakini kulingana na kazi yangu na status yangu nje mashabiki zangu wanapenda nizidi kupendeza unapochuja anakuponda huyu naye vipi anakutupa kule”.

Lakini pia Linah amezidi kusisitiza kuwa mwanaume huyo awe smart na anajielewa na anajiongeza na pia amesisitiza kuwa kikubwa ni upendo lakini ameweka wazi hawezi kuwa na mwanaume ambaye atamtegemea yeye hata siku moja.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.