Lulu Afunguka Baada Ya Kuvishwa Pete (Video)

Muigizaji wa Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu amefunguka baada ya kufanyiwa bonge la surprise na mpenzi wake ambaye ni CEO wa EFM Majizzo.

Sherehe hiyo iliandaliwa na Majizzo maalum kwa ajili ya watoto wake, lakini mambo yalibadilika ghafla, ambapo wakati sherehe ikiendelea, watoto waliwaita mbele baba ambaye ni Majizzo na Aunt yao ambaye ni Lulu.  Shughuli ya kuvalishwa pete ikafanyika huku Lulu akiangua kilio kwa kutoamini surprise aliyofanyiwa na mpenzi wake huyo.

download latest music    

Lulu ambaye alionekana mwenye furaha kupitiliza amefunguka na kusema engagement hiyo ilikuwa bonge la suprise kwani hakujua kama kutakuwa na jambo kama hilo.

Hii ni video ya mahojiano aliyofanya Lulu mara tu baada ya kuvalishwa pete usiku wa jana:

https://www.instagram.com/p/BoYijxUBZnb/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=yzyk138znv2z

Lulu na Majizzo sasa wameamua kuweka mahusiano yao rasmi baada ya kuishi kwenye mahusiano hayo kwa siri na inaelezwa mipango ya ndoa inafanyika na huenda ikafungwa mwaka huu wakawa mke na mume.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.