Lulu Afungukia Tetesi Za Kubeba Mimba Ya Majizzo

Muigizji wa Filamu za Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu amefunguka na kuanika ukweli wote kuhusu tetesi za yeye kuwa na ujauzito wa mchumba wake Majizzo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Kipindi cha Play List cha mtangazaji Lily Ommy wa Radio Times FM, Lulu amesema kuwa hana ujauzito kama watu walivyodhani, bali alinenepa mno kiasi cha watu kuhisi hivyo kutokana na unene wake kumfanya aonekane kama mjamzito.

download latest music    
Lulu Micheal

Unajua mimi nikinenepa ni asili ya mwili wangu, nina mguu mnene sana hivyo uliongezeka, mwili pia uliongezeka kwa kiasi kikubwa kwani niliongezeka kilo 20 hivyo kila mtu aliamini nina ujauzito, sikuwa na ujauzito”.

Lakini pia Lulu alifungukia Tetesi Za kufunga ndoa walipoenda China  kwa kusema kuwa yeye hajafunga ndoa nchini China kama watu wanavyodai, bali alikwenda kwa ajili ya matembezi tu.

Mimi sijafunga ndoa China kama watu wanavyodai na watu wanaongea kwa sababu sina kawaida ya kutangaza mahusiano yangu“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.