“Lulu Akijishusha Kwangu Akaniomba Msamaha Nitamsamehe”- Mama Kanumba

Mama mzazi wa Marehemu Kanumba ameibuka na kuweka wazi kuwa hana kinyongo na Lulu endapo atakuwa tayari kujishusha na kumuomba msamaha basi atamsamehe.

Lulu alifungwa miezi michache iliyopita baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia marehemu Steven Kanumba aliyekuwa naye kwenye mahusiano kwa kipindi hiko.

download latest music    

Kipindi chote wakati kesi inasikilizwa ni wazi kabisa Lulu na Mama Kanumba hawakuwa katika nafasi nzuri kwani walionekana wakipishana bila kusalimiana na hata Lulu alipohukumiwa kwenda jela Mama Kanumba alisema amefurahishwa.

Mama Kanumba alijiwa juu na watu hasa mashabiki za Lulu ndipo juzi alipofika kuwa hajawahi kumuombea Lulu mabaya na hana tatizo naye kwani alishamsamehe tangu zamani na hana kinyongo naye.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ayo Tv, Mama Kanumba amefunguka na kuweka wazi kuwa endapo Lulu Akitoka jela akaenda kumuomba msamaha basi atamsamehe.

Lulu alihukumiwa na Jamhuri ilikuwa nje ya uwezo wangu iwe nilimsamehe au sikumsamehe sikuwa na uwezo wa kufuta kesi. Mimi sina kinyongo na Lulu alikuja mara ya kwanza nikamsamehe na kama akimaliza kifungo akiwa tayari kwa kuwa yeye ni mtoto mimi mtu mzima kwaiyo yeye anapaswa ajishushe kwangu akiwa tayari akinipmba msamaha mimi nitampokea”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.