Lulu Amekutwa na Hatia Ya Kuua Bila Kukusudia

Muigizaji Lulu Michael aliyekuwa anatuhumiwa kumuua bila kukusudia mpenzi wake Steven Kanumba amekutwa na hatia.

Lulu aliyewasili mahakamani hapo asubuhi ya leo kusikiliza shauri ya kesi yake ambayo ilikabidhiwa kwa baraza la wazee.

download latest music    

Wazee wa Baraza ambao pia ni washauri wa mahakama kuu kanda ya Dar es salaam, wamekubaliana kuwa Lulu ameua bila kukusudia.

Mzee wa kwanza  Alisema:

Nimeridhika na ushahidi uliotolewa kwa pande zote mbili, Elizabeth ameua bila kukusudia kutokana na marehemu kuwa na mwili mkubwa”.

Mzee wa pili pia Alisema;

Naweza kusema kuwa Elizabeth hakuua kimakusudi aliua bila kukusudia”.

Mzee wa tatu pia alimalizia;

Lulu ameua bila kukusudia”.

Baada ya majibu hayo ya baraza la wazee Jaji Sam Rumanyika anategemea kutoa hukumu yake tarehe 13 Novemba mwaka huu.

Bado haijajulikana kwa sheria za Tanzania Lulu atapata hukumu gani mpaka sasa lakini anweza akapata kifungo cha miaka kadhaa jela au hata faini.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.