Lulu Amuhamasisha Ray C Kumrudia Mungu

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Rehema Chalamila maarufu kama Ray C amefunguka na kuweka wazi jinsi video ya msanii wa Bongo movie Elizabeth Michael ‘Lulu’ ilivyomuhamasisha kurudi Kanisani.

Siku chache zilizopita kuna video iliyomuonyesha Lulu kwa mara ya kwanza hadharani kwa ridges yake tangu atoke jela Miezi michache iliyopita kwa msamaha wa Raisi.

download latest music    

Video hiyo ilimuonyesha Lulu akiwa mwenye afya tele kanisani akioenekana akiimba na kumsifu Mungu kwa hisia kali pamoja na waumini wenzake.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ray C aliandika kuwa video hiyo imemfanya akumbuke kipindi cha nyuma wakati alipopitia kwenye matatizo ya kuugua kwani kipindi hicho alikuwa ni mcha Mungu na alikuwa hakosi kanisani tofauti na sasa.

Lulu nimeangalia hii video zaid ya mara kumi nahisi!mpaka machozi yamenilenga kwakweli!Sikumbuki lini nimeingia kanisani.’

Najiona mzima sasa na nasahau kuwa Mungu ni mkali! nimejifunza kitu kutoka kwako my dear! kikubwa sana. You Inspire Me”.

https://www.instagram.com/p/Blpj6psDs1Q/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=seqgtm1xok5m

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.