Lulu Diva Ajitabira Ndoa na Mtoto 2019

Msanii wa muziki wa Bongo fleva ambaye mwaka huu alifanya vizuri na kibao chake cha ‘Ona’ Lulu Diva amefunguka na kusema mwakani ana ndoto ya kuzaa na kuolewa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Lulu Diva amefunguka kuwa kwa kazi yake ya muziki anayoifanya hivi sasa,  kufanya kitu ambacho huko mbeleni hakitampa kikwazo kama kupata mtoto mapema ili akiwa anaendelea kumtafutia maisha, yeye anaendelea kukua.

download latest music    

Ni vizuri sana kujipangia malengo ya kimaisha na mimi ndiyo hivyo nimeshapanga ninachokitaka mwakani kwa sababu maisha yenyewe ni mafupi. 2019 nikifanikiwa kupata ndoa ni heri, lakini hata kama nitapata mtoto nitashukuru pia”.

Mwaka huu ulianza kwa tetesi za Lulu Diva kuolewa lakini taarifa hizo ziliyeyuka Baada ya Lulu Diva kuachwa na mchumba Wake Baada ya kuenea kwa tetesi za mahusiano na Rich Mavoko.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.