Lulu Diva- Kolabo na Rich Mavoko Imebadilisha Maisha Yangu

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na kibao chake cha ‘Ona’ Lulu Abbas maarufu kama Lulu Diva amefunguka na kuweka wazi kuwa wimbo wa Ona umempa mafanikio makubwa.

Lulu Diva aliachia Kolabo hiyo miezi miwili iliyopita aliyomshirikisha msanii anayesemekana kuwa mpenzi wake Rich Mavoko na amepata mafanikio makubwa baada ya utumbo hiyo kufanya vyema.

download latest music    

Kwenye Interview aliyofanya na Global Publishers, Lulu Diva alieleza kwamba nyimbo zake za nyuma zilikuwa ni nzuri na zilifanya vizuri lakini baada ya Wimbo wa Ona, umemfanya atambulike kwenye gemu la Bongo Fleva kama msanii mkubwa na kumpatia shoo za kila mara.

Wimbo wa Ona umenipeleka kwenye levo nyingine kabisa kiukweli. Kwa sasa na mimi ni miongoni mwa wasanii wakubwa, shoo zimeongezeka na hata hadhi pia”.

Kutokana na kufanya vizuri na  wimbo huo Lulu Diva ameonekana kwenye shoo mbali mbali akitumbuiza kama vile In Love and Money Tour ya Vanessa Mdee na Jux hivi karibuni.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.