Lulu Diva Kuchezea Kipigo Kizito Kisa Rich Mavoko

Msanii wa Bongo fleva Lulu Abbas maarufu kama Lulu Fiva anayefanya vizuri na kibao chake cha Ona alichomshirikisha Rich Mavoko amedaiwa yuko mbioni kuchezea kipigo kizito.

Global Publishers wanaripoti kuwa Muigizaji wa kitambo kidogo kwenye filamu ambaye hivi sasa ni mtangazaji wa Redio Times, Ummy Wenslaus ‘Dokii’ ambaye ni dada wa Rich Mavoko amehaidi kumpa kichapo Lulu Diva kama ataendelea kutembea na kaka yake.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Amani, Dokii alisema hajawahi kumpenda mwanamuziki huyo hata kidogo na wala hafikirii kama anaweza kuwa mke bora (Wife Material) kwa kaka yake.

Acha watu waseme mimi mkorofi. Mimi ninayemjua ni wifi yangu ambaye amezaa na Mavoko na si vinginevyo, kiukweli ataniona mimi mtata kwa sababu simuelewi hata kidogo Lulu Diva.

Safari hii nikimkuta kwa kaka yangu Mavoko siwezi kumuacha lazima achezee kichapo changu kama alivyofanya mama Diamond kwa Mobeto maana kiukweli simpendi kabisa Lulu Diva”.

Baada ya povu hilo kwa Dada mtu Gazeti hilo lilimsaka Lulu Diva lilipompa ujumbe huo alimwaga povu hili:

Siwezi kumzungumzia Dokii. Kama yeye kinamuuma basi amkataze Mavoko, kwani mimi nina kosa gani? Mwambie aongee na kaka yake.

Lulu Diva alipoulizwa kama anatumia ndumba kumtengeneza Mavoko hadi kumsahau msichana aliyezaa naye, alisema si kweli kwani mwanamke anayejiamini hawezi kutumia ushirikina katika kumdhibiti mwanaume.

Mimi ni mwanamke ninayejiamini na katika maisha yangu yote sijawahi kutumia kabisa hayo mambo (ya kishirikina), sioni umuhimu wake, mtu akinipenda mimi basi ujue kanipenda jinsi nilivyo na mambo yangu“.

Povu hili la Lulu Diva limekuja baada ya kukataa kata kata kuwa hana Mahusiano ya kimapenzi na RIch mavoko siku chache tu zilizopita.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.