Lulu Hana Utu Wala Ubinadamu Kwa Familia Ya Kanumba, Mange Amtolea Uvivu Lulu

Mchambuzi wa mambo ya siasa Mange Kimambi ameongelea tena kesi ya Lulu safari hii akiweka hisia zake wazi na kusema Lulu ameonyesha jeuri kwa familia ya Kanumba hasa mama yake mzazi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mange amefunguka yafuatayo:

download latest music    

Ngoja niwe mkweli kwanini nimeshindwa kuwa na huruma kwa Lulu, ni sababu alivyoishi maisha yake kwa miaka mitano iliyopita, Hakuonyesha hata chembe ya kujutia kwa kilichotoke hasa kwa familia ya marehemu. Lulu alitakiwa atambue kuwa yeye ndio sababu marehemu hayupo duniani, angeonyesha ubinadamu utu hata kwa Mama Kanumba ambaye alikuwa anamtegemea kwa kila kitu, angalau angemjali yule mama, yote Tisa kumi Lulu kushindwa kwenda makaburini kwaajili ya Kanumba day? hapa ndo nilipomuona huyu msichana hana utu, hivi mtu unaanzaje kuwa na huruma kwa Lulu wakati yeye hana huruma kwa wale aliowasababishia majonzi? Hivi mmewahi kumsikia Lulu anafanya kumbukumbu ya Kanumba?

Mange pia hakuishia hapo aligusia suala la mauaji ya mpenzi wake mwingine aliyefariki baada ya Kanumba, Seki.

Kama Lulu angeonyesha ubinadamu kwa tukio hilo sidhani kama nisingekuwa upande wake ningesema amejifunza kitu, Ila mimi hakina kitu kinaniuma kama Lulu kuishi kama vile hana Deni kwa familia ya Kanumba yaani kama vile wasimghasi, Kanumba angekuwepo leo Mama yake asingekuwa anahangaika na daladala na Bajaji sahivi. Lulu anaenda mahakamani anachekacheka, anapiga picha na watu anachezea Simu kwa furaha yote wakati mama wa marehemu yupo mule ndani? Anapishana na mama Kanumba mahakani bila hats salami hiyo nifair kweli? Mama Wa marehemu yupo pale na majonzi yeye ndio kwanza anaenda pale na staili mpya ya rasta kichwani , kavaa high heels na kupanda migari mikubwa anaenda kumuonyesha mama aliyepauka kwa kupanda daladala tu ambaye mkikaa mnamuombea kwa Mungu? Akitoka mahakamani anaenda kupiga picha anabembea huku anakenua!  Hana utu wala ubinadamu huyo msichana period”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.