Lulu Michael Amehukumiwa Miaka Miwili Jela Kwa Kumuua Bila Kukusudia Kanumba

Siku ya leo muigizaji Lulu Michael aliwasili mahakama kuu kwa ajili ya kusikiliza hatma ya kesi yake ambapa Jaji wa Kesi hi to Jaji. Rumanyika amemhukumu miaka miwili jela.

Jaji Rumanyika aliiambia mahakama katika uamuzi wake amemkuta Lulu na hatia kuwa alimuua Kanumba ingawa hakukusudia kumuua kwa maana ilikuwa ni bahati mbaya ambapo aliongea maneno haya:

download latest music    

Ushahidi wa mazingira ni ushadi ambao mshtakiwa alikuwa kuwa yeye ndio mtu wa mwisho kuwa na marehemu ambapo mshtakiwa alikuwa na marehemu kwa miezi minne, ushadi wa mazingira unaweza kutumika kama msingi pekee wa kumtia hatiani mshtakiwa tena, sasa ninapokwenda kuangalia maelezo ya mshtakiwa kama yanakidhi vigezo nilivyosema awali, pia mshtakiwa katika maelezo yake hakueleza kuwa marehemu alianguka au laah wakati anamkimbiza, maelezo ya dokta Josephine sio maelezo ya cheti cha hospitali hayakuwa na hadhi ya hospitali…”.

Baada ya maelezo hayo Jaji alitangaza kuwa baada ya kupitia ushahidi na maelezo ya pande zote mbili amemkuta mshtakiwa ana hatia ya kuua bila kukusudia na hivyo kumpa kifungo cha miaka miwili jela.

Baada ya hukumu hiyo wakili wa Lulu, Peter Kibatala amefunguka na Kudai Kuwait Wana mpango wa kukataa rufaa juu ya kesi hiyo kwa kile walichodai sio haki kwa hukumu ile.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.