Lulu Michael Atoa Msaada Kutokea Jela

Muigizaji wa Bongo movie Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameguswa na kampeni ya kuchangia pedi kwa watoto wa kike na kutokea gerezani alipo kwa sasa ametoa msaada wake kupitia kwa mtu wake wa karibu Dr. Cheni.

Kituo cha televisheni cha EATV kinaendesha kampeni inayoitwa Namthamini ambayo inakusanya na kupokea michango ya pedi kwa ajili ya kuwapelekea watoto wa kike wa shule mbali mbali ambao hawana uwezo wa kununua pedi.

download latest music    

Mchango huo kutoka kwa Lulu umewasilishwa na Muigizaji wa Bongo movie Dr. Cheni ambaye pia ni mtu wa karibu wa Lulu ambaye amesema Lulu ameguswa sana na kampeni ile na ameamua kutoa kidogo alichoweza kuwa nacho.

Kwenye mahojiano na East Africa Tv, Dr. Cheni alizidi kufunguka haya kuhusu mchango huo:

Kwanza niwapongeze kwa hii program nimekuwa mfuaatiliaji na naamini itakuwa na ‘Impact’ kubwa kwenye jamii.

Kikubwa mimi Mahsein @drchenitz ni Muwakilishi, nimeleta ‘pic kadhaa za Pads ambazo zitakuwa msaada kwa Wasichana wakitanzania.

Huu ni mzigo wa Elizabeth Michael (LULU), Ameomba niwasilishe kwenu. Nimekuwa nikimtembelea mara kadhaa kumjulia hali na yeye ameomba ashiriki kwenye kampeni hii ingawaje hayupo, yupo (jela)

Zaidi amesema niwaambie ANAWAPENDA saana na anawataka mabint wa kitanzania wawe huru katika kutimiza malengo yao, wasikate tamaa na Mungu atawasimamia”.

Lakini Dr. Cheni alisema tetesi zito zilizokuwa zikisambaa kwa muda sasa kuwa eti Lulu hayupo jela bali alishatoka na kafichwa nchini Uganda jambo ambalo amesema ni tetesi tu mitandaoni.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.