Madee Hana Mpango wa Kufanya Kazi na Warembo.
Msanii wa bongo fleva nchini madee, amefunguka na kusema kuwa hana mpango wa kusimamia wasanii wa bongo fleva wa kike kama wanavyofdanya watu wengine katika lebvel yake.Madee amesema sababu ya kufanya hivyo ni ili kuepukana na usumbufu ambao anaweza kuupata.
“Hapana, sipendi tu mambo hayo namwachia Daxo Chali, ndio anayaweza. Siwezi tu kukaa na watoto wa kike kwa sababu jinsia tofauti tutapishana maneno ataona nimemuonea,” Madee ameiambia Clouds FM.
Madee ameongeza kuwa kila siku hupokea simu zaidi ya 20 za wasanii wakitaka usimamizi chini ya MMB lakini kutokana hawezi kuwasaidia wote huishia kuwashauri. MMB kwa sasa ina wasanii wawili ambao ni Dogo Janja na Gaza