Madee Hana Mpango Wa Kusaini Msanii Wa Kike Kwenye Label Yake

Msanii mkongwe wa Bongo fleva Madee Ali almaarufu kama Raisi wa Manzese amefunguka na kuweka wazi kuwa hana mpango wa kumsaini msanii wa kike kwenye label yake.

Madee ni mmiliki wa label ya muziki inayojulikana kama  Manzese Music Baby (MMB)anayo Mpaka sasa ina wasanii wawili ambao ni Dogo Janja na Gaza.

download latest music    

Madee amefunguka hayo Kwenye Interview na Clouds Fm ambapo amedai sababu pekee ya kufikia uamuzi huoni kuogopa usumbufu unaoletwa na watoto wa kike.

Hapana, sipendi tu mambo hayo namwachia Daxo Chali, ndio anayaweza. Siwezi tu kukaa na watoto wa kike kwa sababu jinsia tofauti tutapishana maneno ataona nimemuonea”.

Kama utakumbuka producer wa muziki kutoka MJ Records Daxo Chali aliingia Kwenye skendo nzito baada ya wadada wawili aliokuwa anawasimamia Nini na Haitham kudai aliwataka kimapenzi na walipomkataa akawatimua.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.