Madongo ya Nay wa Mitego Yawaacha Mtegoni Mashabiki
Tangu kumekuwa na figizu za hapa na pale Katika mitandao ya kijamii msanii Nay wa Mitego amekuwa akitupa madongo gizani bila hata kuwa na uelekeo lakini swali linakuja kuwa madongo hayo yamekuwa yakimlenga nai haswa.
Msanii huyu ni moja ya wasanii ambao mara nyingi wamekuwa wakionywa sana juu ya nyimbo zake za kukosoa sana lakini pia muda wote katika mahojiano na watu amekuwa siku zote akitoa yale ya moyoni bila kuwaza yatamfikia mhusika au la.
Sasa basi tangu kumekuwa na figisu juu ya matamasha matatu mabayo yote yameisha wikiendi hii huku moja likihairishwa kabisa, msanii Nay wa Mitego bado anawatia mashabiki wake kigugumizi hasa kutoka na post zake katika mitandao huku wengi walisema kuwa atakuwa anatafuta bifu na WCB lakini wasafi wamekuwa wakimpotezea hivyo hawajali kile anachoongea.
ikumbukwe kuwa nay wa mitego na diamond waliwahi kuwa marafiki wa muda mrefu na hata kufanya kazi pamoja lakinu ghafla watu hawa walianza kuwa katika