Maimartha Jesse Afunguka Kuteswa na Uzazi

Mtangazaji mkongwe na Muigizaji wa Bongo movie Maimartha wa Jesse amefunguka na kudai hakuna kitu kinachompa kipindi kigumu kwa wakati huu kama uzazi kwani unamnyima kula bata.

Maimartha ambaye hivi karibuni amefanikiwa kujifungua mtoto wake amedai kuwa uzazi unampa kipindi kigumu sana kwani anakuwa anashindwa kutoka na kwenda kula bata kama zamani.

download latest music    

Mai amedai kwa siku hizi chache alizokaa ndani tangu ajifungur kichanga chake amekuwa akitamani japo kuchomoka na kwenda japo kustarehe kidogo lakini imekuwa ni jambo gummy kidogo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Mai amesisitiza kuwa anasubiri kichanga chake kifikishe siku arobaini aanze kwenda kula bata:

Huyu mwanangu ambaye anajulikana kwa jina la Tajiri Mtoto, nitamlea kidijitali kwani nikishamtoa tu arobaini, naanza kujiachia kwa kula bata kama zamani pamoja na kufanya kazi zangu, huyu sitamlea kama yule wa kwanza, kwamba nikae miaka miwili bila kufanya kazi, nikifanya hivyo itakula kwangu maana maisha ya sasa yamebadilika sana, ni lazima mtu ufanye kazi”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.