Majizzo Ampa Tano Diamond na Wasafi Tv

Mkurugenzi na mmiliki wa EFM Radio na TV E, Majizzo amempa pongezi Diamond Platnumz baada ya televisheni stesheni yake ya Wasafi Tv kuanza kufika rasmi .

Siku ya tarehe moja Wasafi Tv ilianza kurysha rasmi matangazo yake Ikiwa ni suala lililosubiriwa kwa hali kubwa na mashabiki wengi ili kuona Diamond Atafanya nini hasa ambacho ni tofauti katika tasnia hii ya burudani.

download latest music    

Majizzo amempa tano Diamond kwa kuwa kijana mdogo kuleta kitu kama hiko ambacho kitasaidia kuleta ajira kwa vijana wengi nchini na pia kuleta changamoto katika sekta a hii ya burudani.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Majizzo alitiririka haya juu ya ujio wa Wasafi Tv:

Ni mpango mzuri uliochukua na mimi binafsi nakupongeza juu ya kuchagua sekta ya vyombo vya habari, kama vijana ni wajibu wetu kuwahamasisha vijana wengine kufanya kazi kwa bidii ili kujenga taifa letu leo na kizazi cha baadae. Sisi kama “E” tumefanya kidogo na tunaamini kuwa Wasafi (TV na Radio) zitafanya mengi zaidi. Karibu tujenge Tanzania.Karibu kwenye tasnia ya habari @diamondplatnumz“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.