Makampuni ya Nguo za Ndani Yalinitafuta Kufanya Matangazo Lakini Nilikataa_Nandy
Mwanadada Nandy siku ya jana alikuwa na mahojiano na waandishi wa habari wa Clouds Media, na baada ya hapo alipata bahati ya kuongea na Millard Ayo ambapo Nandy alifunguka na kusema kuwa makampuni mengi yalimfuata ili kufanya nae kazi hasa ya kutangaza kutangaza nguo za ndani.
Hii ilikuja baadaya nandy kuvujisha video akiwa amevaa nguo ya ndani tu akiwa na mpenzi wake Bilnass hivyo hiyo iliwafanya baadhi ya makampuni kuanza kumsumbua kufanya nae matangazo ya chupi.
Akiongea na millard ayo ,Nandy alisema
watu wa nguo za ndaniwalinitafuta sana,watu wengi sana na kuweka madau tofauti tofaut hadi na pedi walinitafuta pia , lakini siwezi kufanya kitu kama hicho kwa sababu hata kipindi kitu hicho kinatokea sikufanya kama makusudi na nimeniumiza sana na kipo moyoni bado mpaka sasa.siwezi kuchukulia ilo kama fursa na mimi nikakaa na nikaanza kutangaza jamani chupi hii ni kama yangu.
Nandy anasema kuwa hawezi kufanya hivyo kwa ajili ya pesa kwa sababu ana vyanzo vingine vya kumpati apesa labda miaka mitano mbeleni kama mtu ataona kuwa chupi yake itampendeza ndipo atafanya baishara ya matangazo a chupi lakini sio sasa hivi.