Mama Diamond Athibitisha Kumpa Kipigo Cha Mbwa Mwizi Hamisa Mobetto

Mama mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi. Sandra au maarufu kama Mara Diamond amethibitisha kumpa kipigo cha mbwa mwizi mkwe wake Hamisa Mobetto.

Mwanzoni mwa wiki hii kuna stori ilisambaa kuwa Mama Diamond kampa kipigo kizito Hamisa baada ya Kumekuwa nyumbani kwa Diamond Madale hadi kuacha wigi lake.

download latest music    

Mama Diamond amethibitisha habari hizo kwenye mahojiano aliyofanya na Globa Publishers ambapo ameweka wazi kuwa hampendi na hataki hata kumuona nyumbani kwake:

Ni kweli nilimpiga na wigi nikamvua na hayo  mambo ya kumfuata mzazi mwenzie ni huko, pale Madale ni kwangu na simtaki nyumbani kwangu kabisa.

Mama Diamond aliulizwa sababu gani hasa ilimfanya amchukie Mobetto na alifunguka haya:

Kitendo cha kuniitia mimi Shilawadu (kipindi cha udaku cha Televisheni ya Clouds) kilinikera sana halafu nikaanza kutukanwa kwenye mitandao ya kijamii.

Lakini pia Mama Diamond aliweka wazi kuwa baada ya kumtembezea kipigo Hamisa alimvua wigi ndipo Diamond alikuja kumuamulia:

Mama Diamond ameweka wazi hamtaki Mobetto na  kama mwanaye atakuwa na Mahusiano naye basi hawataelewana:

Kwanza tu siyo mwanamke wa kuoa (wife material) hajui kutandika hata kitanda wala kufanya tu usafi ni shida.

Yaani atajua yeye mwenyewe maana mimi ndiyo nimemzaa Diamond na siyo yeye sasa sijui nani ana nguvu hapo.

Siwezi kukanyaga kwenye  harusi yao hata siku moja watasherekea wenyewe”.

Mama Diamond ameweka wazi kuwa anataka Mwanayr amletee mwanamke mwingine anayejiheshimu na sio Mobetto.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.