Mama Kanumba Afunguka Kuhusu Picha za Nabii Tito na Mwanae

Mama wa marehemu Steven Kanumba amefunguka baada ya kusambaa kwa picha za Nabii Tito na mwanae maraehemu steven kanumba  miaka ya nyumba kipindi cha uhai wake.Mama huyo amekiri  kuwa mwanae alishawahi kukutana na nanbii huyo lakini nia yake iligonga mwamba.

Mama Kanumba anasema kuwa nabii tito alikutana na Kanumba na kumuomba ajiunge katika kanisa lake alilokuwa amelianzisha kwa niaba ya kuwavutia watu watakaokuwa wanakuja kwa ajili ya kumshangaa Kanumba   lakini kwa upande wake itakuwa faida kwa sababu atakuwa amejaza watu.

download latest music    

Mama Kanumba anasema kuwa marehmu Steven alikataa kata kata kuhusu ombi hilo kutokana na imani yake haukumtaka kufanya hivyo lakini pia Kanumba hakutaka kuhama kanisa analosali hata siku moja.

Kwa upande wa Seth ambae ni mdogo wake na marehemu Kanumba ambae poia kwenye pia hizo amekuwa akionekana amesema kuwa ni kweli Nabii Tito aliwahi kuja ofisini kwa kaka yake zilizopo Sinza-Mori kipindi hicho kaka yake alikuwa hai na kuwashauri wahamie katika kanisa lake lakini walikataa na ndipo alipowaomba wapige nae nae picha.

Tabii tito ni mkazi wa Dodoma alieibuka kama nabii huku akihubiri neno la Mungu kwa kutumia biblia lakini akisapoti unywaji wa pombe kanisani na kuwa kuoa mwanamke zaidi ya mmoja ni swala halali huku alishauri hata kuona wasaidizi wa ndani pia ni sahihi.

Nabii Tito aliendelea kupata umaarufu baada ya kumuomba msanii Wema Sepetu kusali katika kanisa lake na pia aweze kumuoa ilhali yeye mwenyewe akiwa na wake watano na watoto 12, nabii tito alimuona wema aje katika kanisa lake ili aweze kupata idadi kubwa ya wafuasi kwa kuwa watakuwa wanakuja kumshangaa yeye kanisani.

Mpaka sasa Nabii Tito amekamatwa na kufanyiwa vipimo ambapo alikutwa na magonjwa ya akili na kuanza matibabu lakini pia kesi yake ikiendelea mahakamani, kosa kubwa  la Nabii huyo kufanya mahubii ya dini ya kikristo kwa kutumia msalaba na biblia kinyume na taratibu za kanisa.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.