Mama Kanumba Amwagia Povu Zito Wema Baada Ya Kugoma Kuigiza Naye

Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu alifunguka hivi karibuni na kuweka wazi kuwa miaka ya nyuma wakati yupo Kwenye Mahusiano na Marehemu Steven Kanumba alimwambia hataki mama yake aigize.

Tangu Kanumba aage dunia miaka michache iliyopita mama yake mzazi na yeye ameingia Kwenye sanaa ya Bongo movie na hivi sasa ameshaigiza Movie kadhaa.

download latest music    

Siku chache zilizopita Wema Sepetu alifanya mahojiano na Global Publishers ambapo aliulizwa kama atakuwa tayari kushirikiana Kwenye filamu na Mama Kanumba ndipo Wema alitoboa kuwa hawezi kwa sababu  Kanumba alikataa mama yake kuigiza.

Baada ya taarifa hizo kusambaa Mama Kanumba ameibuka na kumtolea povu zito Wema na kudai kuwa sababu pekee ambayo ilimfanya mwanaye amkataze kucheza filamu ni kwa sababu alikuwa anamuangalia yeye na kumtunza lakini hivi sasa hana msaada hivyo inatakiwa aigize.

Kanumba alisema hayo kwa kuwa alikuwa ananitunza yaani ananinunulia vyakula na kunilipa mshahara kila mwezi kama mfanyakazi lakini sasa hayupo, je Wema alitaka nishike bakuli nikaombe barabarani au? Maana kulima siwezi hivyo naona tu bora niigize ili niweze kujikimu kimaisha”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.