Mama Kanumba Asononeshwa na Kitendo Cha Lulu Kutolewa Jela Mapema

Mama mzazi wa aliyekuwa muigizaji wa Bongo movie Steven Kanumba, Florah Mtegoa maarufu kama Mama Kanumba ameeleza machungu yake baada ya Lulu kuachiwa gerezani jana.

Siku ya jana Jeshi la Magereza lilitangaza rasmi kuwa Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameachiwa rasmi kutoka gerezani baada ya kukaa ndani kwa miezi mitano ambapo alitajwa kwenda kuendelea na kifungo chake nje.

download latest music    

Tangu Lulu afungwe Mama Kanumba aliweka wazi kuwa alifurahia kifungo cha Lulu na hata kudai kuwa kifungocha miaka miwili kilikuwa kidogo kwa mauaji ya mtoto wake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na MCL digital, Mama Kanumba amefunguka kuwa tangu amepata taarifa kuwa Lulu ameachiwa amekuwa akikosa usingizi na hata presha kupanda kwani ameumizwa sana na taarifa hizo.

Tangu nilipopata taarifa hizi nimejikuta nakosa usingizi na kuumwa presha hivyo leo imenibidi niende kwenye maombi kwa ajili ya afya yangu.

Lakini siku zote naamini Kuwa maskini hana haki”.

Lakini Mama Kanumba amewashukuru wote walioshiriki katika kumtoa na kuongeza kuwa anaamini hiyo yote ni kwa sababu yeye hana hela.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.