Mama Kanumba Ateta na Mh Mwakyembe
Mama mzazi wa marehemu steven kanumba amempongeza mh mwakyembe kwa hatua yake anayotaka kuichukua kuhusu kupitia mikataba ya wasanii ambao walikuwa wakisaini mikataba ambayo inaonekana haiwanufaishi walengwa au ndugu wa baadhi ya mastaa ambao ni marehemu.
Amesema kuwa hatua hiyo ni nzuri na muhimu kwake kwani amekuwa akiona kazi za mwanae kila siku mitaani lakini yeye hakuna anachonufaika nacho.
“Kwangu mimi ni faraja, namshukuru Waziri Mwakyembe kwa kuliona hilo. Kwa mfano mwanangu Steven Kanumba, movie zake naziona lakini mama yake ni masikini wanaofaidi ni wengine, sasa kupitia hilo tamko la serikali nasema asante Mungu,” amesema.
“Mimi ni staa nisiye na hela, kazi za mwanangu naziona tu mtaani lakini mimi ni maskini,” Mama Kanumba ameiambia Clouds TV.
Wiki iyopitia Bungeni wakati wa mjadala wa bajeti ya wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa mwaka wa fedha 2018/19, Waziri Dkt. Harrison Mwakyembe alisema ameunda kamati ya wanasheria ya kuchunguza mikataba ya kibiashara waliyoingia marehemu Steven Kanumba na Mzee Majuto