Mama Kanumba Kuifufua Kampuni Ya Kanumba Iliyokufa Baada Ya Kifo Chake

Mama mzazi wa aliyekuwa staa wa Bongo movie Marehemu Steven Kanumba, Florah Mtegoa ameweka wazi nia yake ya kuirudisha sanaa katika ramani miaka baada ya kifo cha mwanaye kwa kuifufua kampuni yake iliyokufa baada ya kifo chake.

Mama Kanumba amefunguka na kusema baada ya kifo cha mwanaye huyo alidhani huenda mtoto wake mwingine, Seth Bosco angeweza kuvaa viatu vya kaka yake na kuiendeleza sanaa lakini amevishindwa.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers,Akipiga stori na Star Showbiz, mama Kanumba alisema kuwa

Baada ya kifo cha mwanangu Kanumba ukweli kila kitu kilivurugika si unajua muanzilishi ni muanzilishi tu nikajua mimi na mwanangu Seth tungeweza kuindeleza lakini baadaye tulishindwa maana Seth alishindwa kuvaa viatu vya marehemu kaka yake kama nilivyotegemea.

Lakini naomba niwaambie kwamba tuko kwenye michakato ya kuifufua kampuni hiyo baada ya kuzisoma chalenji nyingi za tasnia hii ambapo awali sikuwa na uzoefu kama nilionao sasa”.

Baada ya kifo cha Kanumba, Mama Kanumba na yeye alijiingiza kwenye fani hiyo ya kuigiza ingawa amewahi kukiri kuwa mwanaye hakutaka kabisa kumuona akiwa anaigiza lakini anafanya hivyo kwa hivi sasa ili kuingiza kipato.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.