Mama Kanumba: Lulu Angeachwa Atumikie Kifungo Kidogo

Mama mzazi wa aliyekuwa Muigizaji wa Bongo movie Steven Kanumba, Florah Mtegoa au na kama Mama Kanumba amesema hajafuraishwa na kitendo cha Lulu kutoka gerezani na anatamani angeachwa atumikie kifungo kidogo tu.

Lulu aliyekuwa akitumikia kifungo chake cha miaka miwili katika Gereza la Segerea, alipunguziwa adhabu hiyo Mei 12, mwaka huu kufuatia amri ya Mahakama Kuu huku taarifa ya magereza ikieleza kuwa mrembo huyo, alipunguziwa robo ya kifungo chake kutoka kwenye msamaha wa Rais Dk John Pombe Magufuli.

download latest music    

Lakini pamoja na watu wengi kufurahishwa na kitendo cha Lulu kuachwa huru lakini Mama Kanumba ni mtu mmoja ambaye hakupenda hata kidogo kitendo hicho ambapo Kwenye mahojiano na  Global Publishers alifunguka haya:

Najua Lulu na ndugu zake wanasherehekea sasa hivi lakini wakae wakijua sijafurahishwa na kilichotokea. Kanumba alikuwa akiwalipia kodi Lulu na mama yake lakini leo wanafanya haya wanayoyafanya kweli? Bora hata wangemuacha atumikie kidogo adhabu lakini namuachia Mungu”.

Baada ya kutoka jela Lulu ameendelea na kifungo cha nje ambapo ameonekana akiw anafanya usafi katika wizara ya mambo ya nje kama muendelezo wa kifungo chake cha nje.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.