Mama Kanumba: Natamani Kwenda Kumuona Lulu Gerezani

Mama mzazi wa aliyekuwa msanii wa Bongo movie Marehemu Steven Kanumba, Mama Kanumba ameibuka na jipya tena huku safari hii anatamani kwenda jela kumuona Lulu.

Mama Kanumba hakuwa na uhusiano mzuri na Lulu kwani mpaka a nafungiwa walikuwa kama wana ugomvi fulani huku Mama Kanumba alidai sababu kubwa ni Lulu kumtupa mama huyo na kutomjali kwa lolote.

download latest music    

Miezi michache iliyopita Muigizaji wa Bongo movie Lulu Michael alifungwa gerezani kwa miaka miwili baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa mpenzi wake Steven Kanumba.

Baada ya Lulu kufungwa Mama Kanumba hakusita kuonyesha furaha yake juu ya Lulu kufungwa na baadae alipoulizwa endapo ana mpango wa kwenda kumtembelea Lulu gerezani alisema hajui mpaka afanye mazungumzo na Mungu wake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Mwananchi Communications, Mama Kanumba ameibuka na kusema anatamani kwenda kumuona Lulu jela:

Tangu Lulu kahukumiwa nimekuwa nikipokea lawama na watu kunitusi kuwa mimi ndio sababu, na kusahau ya the kwamba mimi nilishamsamehe kama binadamu na siye niliokuwa mlamlamikaji katika kesi hiyo isipokuwa alishitakiwa na serikali”.

Lakini Mama Kanumba amesisitiza kuwa yote yaliyotokea anamuachia Mwenyezi Mungu kwani yeye kufungwa hakuwezi kumrudishia mtoto wake ambaye amekwisha tangulia mbele ya hali.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.