Mama Kanumba- Siwezi Kuhudhuria Harusi Ya Lulu na Majizzo

Mama mzazi wa aliyekuwa msanii wa Bongo Movie Steven Kanumba, Florah Mtegoa ‘Mama Kanumba’ ametoa povu zito hivi karibuni baada ya kuulizwa Kuhusu Ndoa ya Lulu na Majizzo.

Kwa wiki kadhaa sasa kumekuwa na tetesi kuwa muigizaji wa Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu na mpenzi wake Majizzo wanatarajia kufunga ndoa hivi karibuni.

download latest music    

Mama Kanumba amefunguka kuwa, endapo atapelekewa kadi ya mwualiko wa harusi hiyo hawezi kwenda kwa sababu tangu atoke gerezani hawajawahi kuonana na Lulu wala kusalimiana naye.

Kwenye mahojiano na Ijumaa Wikienda, Mama Kanumba amedai kuwa, hata hiyo habari yenyewe ya Lulu kuolewa na Majizo anaisikia kwenye vyombo vya habari na kwamba hajui lolote.

Kwanza hiyo habari yenyewe nimeisikia kwenye vyombo vya habari, lakini mimi sijui kabisa kama wanaweza kuniletea hiyo kadi ya mwaliko na hata wakiniletea siendi.

Najua itakuwa ngumu tu katika mazingira tuliyopitia sisi, kwanza mimi sasa hivi muda mwingi ninajikalia nyumbani tu kutoka na maradhi yangu haya presha”.

Mama Kanumba aliweka wazi kutofurahishwa na kitendo cha Lulu kutoka jela mapema baada ya kupata msamaha wa Raisi na kupewa kifungo cha nje mapema mwezi uliopita.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.