Mama yake Lulu Elizabeth Micheal adai kuwa hataki kutajiwa mambo na harusi ya mwanae tena

Mama Lulu, Lucresia Karugila amedai kuwa hataki waandishi wa habari kushinda wakimsumbua na suala la ndoa ya mwanae. Mama huyu ambaye hakuoneka kuwa na furaha alisema haya baada ya mwandishi mmoja wa Global publishers kujaribu kujua kikao cha harusi hiyo kimefika wapi.

Mama Lulu

Lucresia Karugila anasemekana kuwa alidai kuwa hana kitu cha kusema kuhusiana na ndoa ya lulu kwani hakuna anayetaarifa za kudhibitisha kuwa mwanae anaoleka na alikyekuwa mpenzi wa Hamisa Mobeto, Majay.

download latest music    

Mama huyo aliendelea kudai kuwa amechoswa na suala hili na kwa sasa hataki kuhusishwa na mambo ya kijinga. Mazungumzo yake na mwandishi huyo yalienda hivi.

Amani: Mama nataka kujua nini kinaendelea kwenye vikao vya mwisho vya harusi ya Lulu na ….(akitajiwa jina
la mchumba wa Lulu), wewe kama mama unasemaje?

Mama Lulu: Sitaki kabisa, kwanza una mama wewe? Sitaki kusikia ukinifuatilia na nilishakuambia tangu zamani, sitaki uniulize mambo ya kijinga kama hayo, hayanihusu kwa vyovyote, tena nisikusikie
kabisa, niache nifanye mambo yangu ya msingi, unasikia? Achana na mimi, tiiiii….titiiiiii (akakata simu).
Jitihada za kumpata Lulu kwa lengo la ufafanuzi juu ya jambo hilo la heri ziligonga mwamba kufuatia simu yake kutokuwa hewani hivyo jitihada bado zinaendelea.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua