Maneno ya Nikki wa Pili Kuhusu Upendo na Mahusiano.

Msanii wa bongo fleva kutoka kundi la Weusi nchini , Nikki wa Pili ambae amekuwa ni moja ya wasemaji wazuri sana hata kuwasemea vijana kuhusu maisha wanayoishi na kutoa manen mengi ya hamasa na kujenga kwa vijana , siasa na hata katika maswala ya uchumi amefunguka na kuweka wazi kuhusu kile anachokifikiria kuhusu upendo na mahusiano.

Nikki ambae mara yingi katika nyimbo zake amekuwa akitoa maneno yanayoumiza moyo hasa kwa vijana kama unaishi yale maisha aliyoimba katika nyimbo zake , amekuwa ni moja ya wasanii aanependa kutoa ukweli kuhusu wasichanaau vijana wanaojiingiza katika mahusiano bila kujua dhumuni la mahusiano hayo au ambao wapo kimaslahi zaidi.

download latest music    

upendo ni msaada , kusaidiana katika uchokoraa wenu na tabia zenu, ulemavu wa matendo yenu  na uyatima wa mioyo yenu.

upendo ni uvumilivu kupeana muda wa kutambuana na kurekebisha makosa,muda wa kukua na muda wa kujifunza.

upendo ni msamaha, kujisamehe mwenyewe kwanza ili usiwe na sumu ndani yako na kumrekebisha mwenzako.

upendo ni ndoto na maono.kuota maisha ya mwenzakoalivyozaliwa,kukua na kujua kwanini yuko vile alivyo.upendo sio kumpenda kama unavyojipenda kwa sababu hata wewe uanamambo yako mengi usiyo yapenda, so ukimpenda kama unavyjipenda yale usiyoyapenda kwako pia hutayaenda kwake…upendo ni ahadi ya kuendelea kuwa mkarimu hata kwa mambo yanayokuwa ndimu.

Nikki wa Pili yuko katika mahusino ya kimapenz na mwanadada mmoja ambae amekuwa akiweka picha zake katika ukurasa wake wa instagram kwa muda mrefu.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.