Mange Afunguka Kuhusiana na Ugonjwa Uliompata Hamisa na Kumpa Shavu Baada Ya Kushinda Tuzo

Mshawishi wa mambo ya siasa mtandaoni, Mange Kimambi ameibuka na kumtetea mrembo Hamisa Mobetto baada ya kugubikwa na skendo baada ya kusemekana amechanganyikiwa.

Tangu wiki iliyopita habari zilienea mtandaoni kuwa mzazi mwenxie na Diamond, Hamisa Mobetto amechanganyikiwa na kile kilichohusishwa na Imani za kishirikina huku watu wengi wakidai kuwa Hamisa ametupiwa uchawi na hivyo kusababisha yeye kuwa kama chizi.

download latest music    

Jana kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mange alifunguka kuwa habari za Hamisa kuchanganyikiwa kwa kulogwa zinasambazwa na maadui tu bali ukweli ni kuwa Hamisa alikuwa anaumwa malaria:

Hamisa alipatwa na malaria kaliii ikapanda hadi kichwani, ila hadi hivi sasa anaendelea vizuri. Hizi stori za kuwa amegeuka chizi and so forth ni chumvi tupu zimeongezwa…..But its true alikuwa anaumwa na ishu ni malaria kali ambayo ilipanda kichwani, ila sasa hivi anaendelea vizuri tuendelee kumuombea”.

Pia Mange alimpongeza Hamisa kwa kushinda tuzo aliyokuwa anagombania na washiriki wengine. Ambapi Mange aliandika

“Hongera kwa kushinda tuzo Toto”

Jana kupitia ukurasa wake wa Instagram Hamisa alitangaza kuwa ameshinda tuzo aliyokuwa anawania;

 

Well…. what can I say? team Hamisa Mobetto we won babies Thank you a guys soo sooo much for your votes Ahsaaanteni saana stardqt awards thank you babies, Ila nini tuzo yetu kuifuata iko pale pale”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.