Mange: Muda Wowote Wema Sepetu Atatangaza Amerudi CCM

Mwanaharakati wa siasa mtandaoni Mange Kimambi amefunguka na kudai kuwa muigizaji Wema Sepetu na Mama yake mzazi wamerudi CCM.

Wema alihama chama hicho mapema mwaka huu baada ya kukamatwa kwa kutuhumiwa kuuza na kutumia madawa ya kulevya. Baada ya kuachiwa huru Wema aliita vyombo vya habari na kutangaza nia yake ya dhati kabisa ya kuhamia Chadema.

download latest music    

Siku za hivi karibuni kumekuwa na tetesi kuwa Wema anampango wa kurudi CCM ingawa alikataa lakini leo asubuhi Mange kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram alitangaza kuwa Wema amerudi CCM:

Breaking News Wema Sepetu na mama yake wanarudi CCM very soon…Mimi nilijua tu nilipomuona Wema kaenda Rwanda kakacha tarehe ya mahakamani bilauoga nilijua tu kuna mkono wa CCM, kuna mtu Mkubwa CCM aliniletea taarifa kuwa nyumba ya mama Wema inabomolewa wasiporudi CCM wamepewa muda wa kufikiria, na notice ya kubomolewa nyumba wameshapewa. That’s their family house, ila kaniambia mama Wema kashakubali kurudi sahivi anam-convince Wema, kaniambia Wema keshakubali kurudi lakini anaona aibu ni jinsi gani atai-face jamii…yaani unaambiwa mama Wema alivyoambiwa nyumba yake inabomolewa fasta akakubali kurudi CCM. Na kesi kaambiwa akirudi CCM itakwisha vizuri ila akikataa kurudi kila siku atapelekwa mahakamani mpaka arudi na asiporudi anaweza kufungwa”.

Pia Mange aliendelea  kufunguka na kudai kuwa Ana uhakika asilimia 100 kuwa Wema atarudi CCM:

Kilichobaki ni Wema kutangaza tu kwaiyo Watanzanua kaeni sawa muda wowote Wema na Mama yake wanatangaza kurudi CCM na wakisharudi CCM Magufuli habomoi nyumba zao na wakirudi wameambiwa lazima wamsifie na waseme wameona Chadema haifai na yeye ndio anafaa”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.