Mange- Wimbo Mpya Wa Ali Kiba Umebuma

Mwanaharakati wa mambo ya siasa Mtandaoni mwanadada Mange Kimambi amemlipua staa wa Bongo fleva Ali kiba na kusema wimbo wake mpya unaojulikana kama ‘Mvumo wa Radi’ umebuma vibaya mno.

Siku ya Ijumaa Ali Kiba aliachia wimbo wake mpya kwa mara ya kwanza Kupitia kipindi cha XXL ya Clouds Fm lakini wimbo huo umepatwa na masahibu na kudaiwa kufanyiwa figisu figisu na watu wasiojulikana Kwenye mtandao wa Youtube.

download latest music    

Mange ameibuka na kumpa za Uso Ali Kiba kuwa wimbo wake wa Mvumo wa radi umebuma lakini amemtaka asikate tamaa kwani wasanii wengi wanatoa nyimbo na zinabuma na hata akamtolea mfano Diamond na kudai Albamu yake ya A boy From Tandale ilibuma pia.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.