Marehemu Kanumba Alikuwa Ananipiga Kila Siku Akilewa, Amejitetea Lulu Mahakamani

Kesi inayomkabili muigizaji wa bongo movie Elizabeth Michael ‘Lulu’ ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa mpenzi wake na muigizaji Steven Kanumba, bado inaendelea kuunguruma katika mahakama kuu.

Kesi hiyo iliyoanzwa kusikilizwa wiki iliyopita, imeendelea leo mahakamani ambapo kwa Mara ya kwanza Lulu amepanda kizimbani kwaajili ya kujitetea dhidi ya kesi inayomkabili. Asubuhi hii Lulu amejitetea kuwa yeye hakumuua Kanumba bali alidondoka mwenyewe na hakumsukuma kama watu wengi walivyodai. Lulu amesema:

download latest music    

Nilipofika kwa marehemu Kanumba nilimkuta yupo kwenye dressing table, Nilikaa kitandani kwa Kuwait hapakuwa na sehemu ya kukaa, Mara nyingi marehemu alikuwa akilewa ananipiga ila sio kwa akili zake, nilikuwa nataka kutoka na marafiki zangu lakini marehemu alinikataza alikuwa hataki nitoke na marafiki zangu lakini nilipomwambia nataka kutoka na marafiki zangu alinikimbiza mpaka nje akiwa na taulo bila ndala, na mimi nilikuwa naogopa kupigwa alipoona simu yangu inapigwa alihisi ni mwanaume anapiga akasema kwanini naongea na Simu ya mwanaume mbele yake? Marehemu akaingia uvungumi akatoa panga akasema Leo nakuua huku akinipiga na panga kwenye mapaja, Baada ya hapo Marehemu alianguka mwenyewe na kujigonga kwa nguvu na kuinuka sehemu nyingine alikuwa kama anatapatapa, nilivyoona hivyo nilitoka nikaelekea chooni na kupiga makelele Lakini baada ya mufa mchache nilisikia kishindo kama mtu anafungua mlango nilivyorudi nikamkuta amelala nikajua amejiganyisha nikaanza kumwambia watu wakija nawaambia jinsi ulivyonipiga na panga, nilimwambia Seth, akajaribu kumwamsha hakuamka akasema anaenda kumuita  daktari alivyosema hivyo mi nikaogopa nikaondoka nikaona asije akaamka akaanza kunipiga”.

Pia Lulu aliendelea kujitetea;

Niliondoka nikawasha gari nikaelekea coco beach, huko cocobeach sikuenda kuonana na mtu nilenda mwenyewe kutuliza akili yangu Ghafla meseji zikaanza kusambaa watu kuniuliza wa nasikia Kanumba kafariki, nikachukua Simu nikampigia rafiki yake na Kanumba kumuuliza Kanumba amelazwa hospitali gani? Akaniambia usjie hospitali we niambie uko wapi tuonane Bamaga tulivyokutana akawa kama anataka kuongea na mimi lanini ghafla polisi wakaja kunikamata na kunipeleka kituoni Osterbay, nilijua Kanumba kafariki huko huko polisi”.

Pia Lulu amejitetea Kuwa yeye hakusababisha kifo cha  Kanumba bali yeye ndio aliyepigwa na kuumizwa na marehemu  kutokana na yeye Lulu kuwa na umbile dogo lakini pia marehemu alikuwa na panga.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.