Marioo Atangaza Kupanda Bei
Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambae kwa sasa anachipukia na kufanya vizuri katika industry ya muziki MARIOO , amefunguka na kusema kuwa kwa muda amekuwa akiwaandikia baadhi ya wasanii nyimbo na zimekuwa zikifanya vizuri lakini anadhani kwa sasa ni muda muafaka wa yeye kuanza kufanya kazi hiyo kwa mafunaa yake zaidi.
Marioo anasema kuwa jatoacha kuandika nyimbo bora, lakini anadhani kuwa atakuwa akiandika nyimbo nzuri kwa kulipwa ili na yeye aanze kuapata thamani ya kile anachokifanya.
Akiongea na Clouds Media, Mario anasema “Sijasema naacha kuandikia nyimbo apana, bali nitaendelea kuandika nyimbo lakini sio kama zamani kwa sasa nitataka mtu anilipe ndio tufanye kazi ili na mimi nipate thamani kama mwandishi.”
Wasanii wengi wamekuwa waandishi wa nyimbo za watu wengine lakini wamekuwa hawanufaiki na uandishi wao pamoja na kwamba nyimbo hiyo inaweza kufanya vizuri mpaka kimataifa, na kwa Tanzania wasanii wamekuwa wakgumu sana kuwek a wazi kuwa wanaandikiwa nyimbo na wasanii wenzao na kuwa-acknowledge.