Marioo Atangaza Kupanda Bei

Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambae kwa sasa anachipukia na kufanya vizuri katika industry ya muziki MARIOO , amefunguka na kusema kuwa kwa muda amekuwa akiwaandikia baadhi ya wasanii nyimbo na zimekuwa zikifanya vizuri lakini anadhani kwa sasa ni muda muafaka wa yeye kuanza kufanya kazi hiyo kwa mafunaa yake zaidi.

Marioo anasema kuwa jatoacha kuandika nyimbo bora, lakini anadhani kuwa atakuwa akiandika nyimbo nzuri  kwa kulipwa ili na yeye aanze kuapata thamani ya kile anachokifanya.

download latest music    

Akiongea na Clouds Media, Mario anasema “Sijasema naacha kuandikia nyimbo apana, bali  nitaendelea kuandika nyimbo lakini sio kama zamani kwa sasa nitataka mtu anilipe ndio tufanye kazi  ili na mimi nipate thamani kama mwandishi.”

Wasanii wengi wamekuwa waandishi wa nyimbo za watu wengine lakini wamekuwa hawanufaiki na uandishi wao pamoja na kwamba nyimbo hiyo inaweza kufanya vizuri  mpaka kimataifa, na kwa Tanzania wasanii wamekuwa wakgumu sana kuwek a wazi kuwa wanaandikiwa nyimbo na wasanii wenzao na kuwa-acknowledge.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.