Martin Kadinda Ajikanyaga Kuhusu Penzi La Wema na Diamond

Mbunifu wa mavazi na mwanamitindo maarufu nchini Martin Kadinda ambaye pia anajulikana hasa kwa kuwa Meneja wa Muigiaji wa Bongo movie Wema Sepetu, amejikuta katika wakati mgumu na kujikanyaga alipoulizwa kuhusu hali ya penzi la Wema Sepetu na Diamond Platnumz.

Wiki iliyopita aliyekuwa Staa Diamond Platnumz aliachana rasmi na mpenzi wake Zari na hivyo kuacha nafasi ya watu kujaza nani atakuwa na Diamond kwa hivi sasa na moja kwa moja kila mmoja alielekeza macho yake kwa Wema.

download latest music    

Wema na Diamond wamekuwa wakitawala headlines mbalimbali kwenye social media wakidaiwa kuwa wamerudiana huku kitu kikubwa kilichosababisha hiyo yote ni baada ya Wema kuonekana akikumbatiana na Diamond hadharani.

 

Diamond na Wema wiki chache zilizopita

Martin sio tu alikuwa meneja wa Wema bali pia ni rafiki wa karibu kwaiyo kutokana na ukaribu alionao na Wema gazeti la Amani lilimtafuta na kumuuliza endapo hizi tetesi zinasombaa kuwa Diamond na Wema kurudiana zina ukweli wowote m? Cha ajabu Martin alijikanyaga sana kujibu swali hili mwishowe alisema;

Jamani mimi siwezi kuzungumzia lolote kuhusu hilo na hata sijui nianzie wapi kuzungumza lakini kama ishu nyingine yoyote nitazungumza kwa mapana yote lakini sio suala hilo hata kidogo kwa kweli”.

Martin aliulizwa swali hilo kwa sababu siku ya tukio la Diamond na Wema kukumbatiana na kupeana busu wiki chache zilizopita Martin naye alikuwepo na alionekana kuongea na Diamond Pamoja na Wema.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.