Mashabiki Wahoji Mahusiano ay WCB na Zamaradi.

Mtangazaji wa zamani wa Clouds Media Group, Zamaradi Mketema ambaye baada ya kuvunjika kwa mahusiano yake ya kimapenzi na Mkurugenzi wa CMG, Ruge Mutahaba, alihamia Wasafi Media kuendelea na career yake.

Baada ya uzinduzi rasmi wa Wasafi TV na Wasafi FM, ilitarajiwa mtangazaji huyu mahiri kuanza kuonekana kwenye runinga akiendesha kwa mafanikio kipindi kama alivyokuwa akifanya Take One na kituo chake cha kazi cha zamani.

download latest music    

Tofauti na matarajio ya wengi, ghafla mwanadada Zamaradi ameanza kujiondoa kushiriki kwenye kazi zote zinazohusiana na Wasafi pengine kabla hata ya kuanza. Na kwa tukio la hivi karibuni la Wasafi Festival, hakuonekana kuongelea chochote kama ilivyo ada kwenye projects nyingine za Mwajiri wake huyo mpya.

Sasa, kwa sababu bado hakujatoka official say, naomba kupitia uzi huu tukajaribu kudodosa endapo kuna lolote linaloendelea linalopelekea awe kimya kabisa huku akionekana kuwa busy na shughuli zake nyingine.Maswali ya shauku;

1. Mgongano wa kimaslahi na kukomoana baina ya Wasafi Media na Clouds Media umemweka njia panda?
2. Hali ya Afya ya mzazi mwenzie (Ruge) imemfanya ashindwe kuvumilia kuhimili vishindo vya kejeli kutoka kwa wanaofurahia anguko lake?
3. Ameshindwana malipo na Wasafi Media?
4. Anaamua kuwa freelancer?
5. Ana mpango wa kurudi Clouds Media Group?

Hayo ni miongoni mwa maswali yamekuwa yakiulizwa na mashabiki katika kurasa nyingi za udaku huku wakitaka kujua kwa hamu juu ya swala hlo ingawa pia  moja ya watu wanaopenda kufatilia mambo katuka mitandao dada Mange Kimambi alisema katika mojaya majibu ya mashabiki kuwa zamaradi tayari ameshindwa kuelewana kikazi na WCB hivyo ameona ni bora kuachana nao tu.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.