Mashabiki Wamliza Diamond Cheni ya Milion 40
Mashabiki wa msanii Diamond katika mkoa wa Mtwara wamemliza msanii wao baada ya kumkwapua cheni ya shiling milion 40 ikiwa shingoni mwake baada ya kuvua bila ya yeye mwenyewe kujijua siku ya kuwasili mtwara.
Diamond ambae alionekana akiwa ma shamrashamra za kupokelewa na mashabiki zake huku akizunguka nao katika kila mtaa mkoani Mtwara aamesema alivaa cheni hiyo lakini hakujua kama linaweza kutokea lolote kama hilo lakini kwa sababu ni mashabiki hakuna namna wanaweza kuitafuta tena.
Diamond alikuwa Mtwara na timu yake kwa ajili ya kufanya show iliyozinduliwa wikiendi hii na kuanza kufanyika karibia mikoa yote ya Tanzania.