Mashabiki Wanataka Niwe na Nandy – Aslay

Mwanamuziki mkali wa Bongo fleva Aslay Amefunguka na kudai kuwa mashabiki zake wengi wanafurahia akifanya kazi na msanii mwenzake Nandy hivyo wanataka awe naye.

Aslay ambaye amekuwa akifanya vizuri kwenye ulimwengu huu wa muziki wa Bongo ambapo ni mara kwa mara amekuwa akishika chati ya juu kwa nyimbo zake. Aslay alitokea kwenye kundi la Yamoto band lakini tangu ameanza kufanya muziki kama solo artist amepata mafanikio zaidi.

download latest music    

Siku ya Jana Aslay na Nandy wameachia wimbo wao mpya unaoitwa ‘SubalKheri mpenzi’ wimbo huu ukiwa wa pili amemshirikisha Nandy Aslay amesema mashabiki zake wanawasababisha wafanye hivyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Planet Bongo ya East Africa Radio, Aslay amesema kuwa mashabiki zake walifurahia pale alipofanya kazi ya kwanza na Nandy na ndipo walipoona ni vyema wakarudi tena studio kufanya kazi nyingine kwa ajili yao:

Ni pendekezo la mashabiki tumeona mashabiki zetu wakitaka kitu kingine kutoka kwetu baada ya kazi ya kwanza na Nandy inaelekea mashabiki wanapenda kuniona na Nandy hivyo tukaona tuingie jikoni tuwapikie kazi mpya”.

Aslay tangu awe solo artist ametoa jumla ya nyimbo kumi na sita ambazo amesema ilibidi atoe nyimbo nyingi kwa wakati mmoja ili aweze kupiga nyimbo zake mwenyewe kwenye shoo zake bila kutegemea nyimbo alizokuwa anaimba wakati yupo Yamoto.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.