Mashabiki Waombwa Kumsaidia Hawa wa Nitarejea
Kama mwaka sasa umepita tangu mwanadada hawa alipowahi kutolewa katika vyombo vya habari kuwa alikuwa amekuwa kama teja kutokana na matumizi ya pombe za kienyeji zilizompelekea pia kuacha muziki na kujikuta akibaki nyumbani tu,
Baada ya hapo walimsaidia dada huyo na kwenda sober ambapo alipatiwa matibabu na kuanza kurudi katika hali yake ya kawaida lakini bado alikuwa akihitaji msaada wa hapa na pale ili kurudi kimuziki.
Sasa mapya ayameibuka kuhusu hali ya mwanadada huyu huku akionekana kuendelea kudhoofka kabisa na hii yote ni kutokana na ukweli kuwa mwanadada huyo kwa sasa ni mgonjwa sana na amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa ini unaoendelea kutafuna sana afya yake.
Soudy Brown wa kipindi cha shilawadu kutoa Clouds Media amethibitisha ilo baada ya kwenda kumtembea mwanadada huyo huku akionekana kudhoofika sana na hali yake aliyonayo kwa sasa.
Mwanadada huyo anaomba msaada kwa watu mbalimbali kwa chochcote kwa sababu ya matibabu na pia hata familia yao pia haina uwezo kwa kutoa huduma ya kila kitu.