Mastaa Wapunguze Kudanga Waige Mfano Wa Lulu- Sabby Angel

Msanii wa muziki wa Bongo fleva na Bongo Movie Sabrina Omary maarufu kama Sabby Angel amefunguka na kusema anamkubali sana Lulu na ni mfano wa kuigwa na kuwataka mastaa waige mfano wa Lulu.

Kuanzia Siku ya Jumapili Lulu ametawala headlines zote baada ya kuvalishwa pete ya uchumba  na mpenzi wake wa siku nyingi ambaye ni CEO wa EFM, Majizzo.

download latest music    

Sabby Angel  amefunguka na kumpongeza Lulu kwa jambo alilofanya kwani badala ya kudanga na kuhangaika ametulia na mwanaume mmoja na sasa wapo mbioni kufunga ndoa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Sabby Angel ameandika:

Nimefurahi sana Tena sana kuamka na kuona picha za posa ya Lulu, For real am so happy anaonyesha mwenendo mwema yaani she is a role model. Mwanamke lazima stara. Mastaa wengine wafuate Mfano. Sio kudanga tu na kiki. Kuwa kioo cha jamii lazima uwe Mfano kwani mabinti wengi wadogo hutangalia sisi na kufuata tunayofanya”.

Sabby Angel ametengeneza headlines baada ya kuolewa ndoa yake ya tano baada ya Kuachika mara nne tayari.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.