Maua Sama Afungukia Tetesi Za Kumwagwa na Mzungu

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Maua Sama Amefunguka na kuongelea tetesi zilizosambaa nwneye mitandao ya kijamii kuwa hivi Karibuni ametoswa na mpenzi wake.

Maua Sama ambaye alijizolea umaarufu miaka ya nyuma na ngoma yake ya Amen hivi sasa bado yupo Kwenye gemu na anatamba na ngoma yake ya Iokote ambayo inasikika kila kona.

download latest music    

Pamoja na kufanya vizuri katika muziki wake lakini inadaiwa Msanii huyo hafanyi vizuri sana Kwenye maisha yake binafsi hasa upande wa mapenzi kwani inasemekana Msanii huyo ana ametoswa na mpenzi

Maua ambaye alikuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na mzungu fulani inadaiwa kuwa amejikuta katika kipindi kigumu baada ya kumwagwa.

Kwenye Interview aliyofanya na Global Publishers Maua amekana tetesi hizo na kudai ni maneno ya watu kwani yeye hajaachwa na mtu yoyote:

Hakuna kitu kama hicho. Ujue Wabongo bwana wape picha tu ‘caption’ wataandika wenyewe! Yaani wamejaa kufuatilia mambo ya mtandao na kuyaamini. Kwa sasa nipo katika uhusiano na sipendi kuuweka hadharani“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.