Maumivu ya Penzi la Barakah The Prince Yameisha- Nisha

Muigizaji wa Bongo movie ambaye hivi sasa amegeukia muziki wa Bongo fleva Nisha Jabu amefunguka na kusema maumivu aliyoyapata kutoka na penzi la staa wa Bongo fleva Barakah The Prince yameisha.

Nisha na Barakah The prince walikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi miaka miwili iliyopita lakini penzi hilo liliingia shubiri baada ya Barakah kumtosa Nisha na kuanza Mahusiano na msanii mwenzake mwanadada Naj.

download latest music    

Nisha ambaye ametawala vichwa vya habari hivi karibuni baada ya tetesi kuanza kusambaa kuwa ana Mahusiano ya kimapenzi na Ex boyfriend wa Wolper Brown ambaye ameonekana kwenye video ya wimbo wake wa Bachela.

Ndani ya wimbo huo Nisha amemchana sana Barakah kwa kudai alimfanyia vimbwanga vingi tu enzi za Mahusiano yao ikiwemo alikuwa ana kama kwenye media mbali mbali na kusema hawana mahusiano.

Kwenye Interview aliyofanya na Enews ya EATV Nisha amefunguka mengi juu ya maumivu aliyopata kutoka kwa Barakah na kusisitiza maumivu hayo yameshaisha kwa sasa:

Kuna vitu vingi tu vilivyokuwa vinajiyokeza moja wapo ni kuweza kukanwa kwenye media kuwa hatoki na mimi wakati tunaishi nyumba moja wakati mimi ndio namsapoti na kusapoti kazi yake inafika pale alipo mpaka anajulikana”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.