Mbasha:Tangu Niachane na Mke Wangu Sijawahi Kuzini.

Msanii wa nyimbo za injili  Emmanuel Mbasha amefunguka na kusema kuwa kwa muda mrefu tangu ameachana na mke wake aliekuwa amefunga nae ndoa hajajiingiza tena katika mahusiano ya aina yoyote kwa sababu bado hajapata mwanamke wa kuingia nae katika mahusiano.

Emmanuel Mbasha anasema kuwa   ameamua kuishi bila kuoa  hata kama itamgharimu maisha kwa sababu hata yesu na paulo waliweza kusihi bila kuona na waliweza kuishi.mbasha anasema kuwa pamoja na kwamba yeye pia ni mwanaume aliyekamilika lakini bado amekuwa akimuomba mungu sana kushinda vishawishi vya shetani vya kujiingiiza katika mahusiano hayo.

download latest music    

ukiona niko na mwanamke ujue ni rafiki yangu tu wa kawaida na tangu nimeachana na mke wangu wa kwanza wa ndoa sijawahi kuzini tena,na niko kawaida tu sina matatizo yoyote yale na ukizingatia nafanya sana mazoezi.sina mpenzi wala mchumba kama watu wanavyokuwa wananizushia maneno ya uongo.

Pamoja na kwamba emmanuel amekuwa akikanusha kuwa na mahusiano na mwanamke yoyote lakini hivi karibuni amekuwa akiweka picha katika mitandao ya kijamii akiwa na mwanawake tofauti tofauti na kusemekana kuwa ni mwanamke wake.

Emmanuel Mbasha aliwahi kuwa na mahusiano na msanii wa nyimbo za injili Florah Mbasha kwa na kufanikiwa kuzaa mtoto mmoja lakini baadae walikuja kuachana na kushindwana katika ndoa kwa sababu florah alimfungulia mashtaka kwa sababu ya kisingizio cha kumbaka mfanya kazi wake wa ndani.

 

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.