Mbosso Awakingia Kifua WCB Adai Sio Wanyonyaji Kama Madai Ya Mavoko

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB Maromboso amefunguka na kuwakingia kifua WCB dhidi ya tuhuma za unyonyaji walizotupiwa na msanii Rich Mavoko.

Wiki iliyopita RIch Mavoko aliwaburuza WCB katika Baraza la sanaa Tanzania (BASATA) na kuwatuhumu kwa unyonyaji kutoka na mkataba waliompa.

download latest music    

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari Mbosso amefunguka na kudai yeye binafsi hajaona unyonyaji wowote WCB  hasa kwa upande wa mkataba wake Tena anaamini wamempa zaidi anachostahili.

Kiukweli kwa upande wangu tangu naingia WCB mpaka leo sijafikisha pesa ambayo wao wali invest kwangu kwaiyo nikiambiwa nanyonywa binafsi nitapinga kwa sababu mimi ndio naona nawanyonya kwa sababu mpaka leo hela waliyowekeza kwangu haijarusi na kuna wasanii wapo WCB mpaka leo pia hawajarudiasha hata nusu ya pesa kwaiyo ukiniambia WCB wananyonya wasanii nakuwa sikuamini labda uje na vigezo”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.